Isaiah 41:11-16


11 a“Wote walioona hasira dhidi yako
hakika wataaibika na kutahayarika,
wale wakupingao
watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.

12 bIngawa utawatafuta adui zako,
hutawaona.
Wale wanaopigana vita dhidi yako
watakuwa kama vile si kitu kabisa.

13 cKwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,
nikushikaye mkono wako wa kuume
na kukuambia, Usiwe na hofu,
nitakusaidia.

14 dUsiogope, ee Yakobo uliye mdudu,
ee Israeli uliye mdogo,
kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana,
Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

15 e“Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria,
kipya na chenye makali, chenye meno mengi.
Utaipura milima na kuiponda
na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.

16 fUtaipepeta, nao upepo utaichukua,
dhoruba itaipeperushia mbali.
Bali wewe utajifurahisha katika Bwana
na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

Copyright information for SwhKC